HUYU MAMA NI MFANO WA KUIGWA KATIKA JAMII; UJASIARIMALI WAKE WAMPA MAFANIKIO
MAMA GODELIVA AKIHUDUMIA MIFUGO
UJASIRIAMALI KWA AKINA MAMA NA AKINA DADA
Kwa majina halisi ninaitwa Godeliva Simon, Ninafanya shughuli ya ujasiriamali
kwa lengo la kujipatia mahitaji yangu mwenyewe pamoja na familia yangu .Ujasiriamali
niufanyao ni wa ufugaji wa Mifugo mbalimbali,mifugo ninayofuga ni kuku wa kienyeji
[Kiswahili],kanga,batamzinga,bata wa kawaida,bata bukini {bata maji},mbuzi wa
kawaida,mbuzi wa maziwa pamoja na sungura. Mifugo hii hunisaidia sana katika
kuongeza kipato badala ya kutegemea mshahara wa mwajiri pekee kwani hali ya
maisha ni ngumu na kila mmoja anaelewa.Nimeanza ujasiriamali huu tangu mwaka
2012 hadi leo hii ninaendelea na ujasiriamali huu wa ufugaji.
Kwa upande wa akina mama pamoja na vijana ninawaomba
mjiajiri kwa upande wa kufuga kwani faida yake ni kubwa, kwa mfano huwezi
kukosa pesa ya matumizi kwa kutumia jasho lako na mikono yako,pia utakuwa na
afya njema kwani hutohangaika kununua yai,nyama na maziwa hususani maziwa ya
mbuzi kama nifaidikavyo mimi,pia utaweza kuepukana na umbea ambao huletwa na
ukosefu wa shughuli za kufanya,
Mafanikio, kupitia ujasiriamali huu umenisaidia kuwasomesha watoto wangu wote, hakika kwangu ni mafanikio kwasababu zawadi pekee kwa mtoto ni elimu tu, pia umeniwezesha kunipatia makazi ya kuishi
Mafanikio, kupitia ujasiriamali huu umenisaidia kuwasomesha watoto wangu wote, hakika kwangu ni mafanikio kwasababu zawadi pekee kwa mtoto ni elimu tu, pia umeniwezesha kunipatia makazi ya kuishi
Ujasiriamali huu kwa njia ya ufugaji una changamoto
mbalimbali ambazo ni
1. Chakula cha mifugo,
hii ni changamoto kubwa kwani ili mifugo ikue na iishi inahitaji chakula
ambacho upatikanaji wake ni mgumu kwani lazima uwe na pesa kwaajili ya
kuwezesha hili, pia chakula cha baadhi ya mifugo kama mbuzi na sungura
upatikanaji wake ni mgumu kutokana na jiografia ya eneo letu hili la dar es
salaam ambalo ni kavu hivyo upatikanaji wa nyasi huwa ni wa tabu sana.
2. Mabanda(makazi)
kwaajili ya kuhifadhi wanyama hawa,
Wanyama hawa wanatakiwa kuhifadhiwa katika mabanda yaliyojengwa vizuri
na imara ili kuwalinda na hali zote pamoja na maadui wa aina mbalimbali, hivyo
pesa nyingi huhitajika ili kukamilisha makazi yao.
3. Soko la mifugo,
inahitajika kama mfugaji uwe na soko la uhakika na si kubangaiza wateja mitaani
kwani hii hupoteza muda na nguvu nyingi.
4. Afya ya mifugo,
mifugo hii huhitaji chanjo ya mara kwa mara ili kuikinga na magonjwa
mbalimbali,mfano batamzinga huhitaji kupatiwa chanjo wiki mbili mara tu baada
ya kutotolewa ili kuwakinga na ndui.
5. Ufadhili,
uanzishwaji wa biashara hii huwa ni mgumu kutokana na ukosefu wa ufadhili
ambapo hukosekana fungu la kutosha kuendeshea biashara hii,ni vyema kabla ya
kuanzisha biashara hii uwe na kianzio(mtaji) wa kutosha,kwa akina mama tulio
wengi tunashindwa kukopa kwani kurudisha pesa hiyo inakuwa ni vigumu kutokana
na ufinyu wa vipato vyetu.
OMBI
Ninaomba akina mama pamoja na
mabinti tuwe tayari kuingia katika
ujasiriamali ili kupunguza utegemezi na pia ukali wa maisha unaotukabili,pia
kwa yeyote anayetaka kujifunza jinsi ya kufuga na kuendesha ujasiriamali huu
ninamkaribisha sana kwa moyo mkunjufu na dhati na kuhusu gharama za mafunzo
haya tutaelewana maana bila kujifunza si rahisi kupata mwamko na kuingia katika
ujasiriamali wa aina hii, pia tuzingatie na kuelewa
kuwa
hakuna lisilowezekana ni vizuri ukawa na nia utafanikiwa.
Kwa
mawasiliano:
Jina : Bi Godeliva Simon
Na.simu:
0784708726
Kauli mbiu
“Mwanamke anaweza ujasiriamali”
MAMA GODELIVA AKIWA KAZINI
Post a Comment